Mbinu za Kukusaidia kuishi kwa Furaha maishani


SABABU ZINAZOWEZA KUKUSAIDIA KUKUJENGA NA KUYAFURAHIA MAISHA.

Katika sehemu ya kwanza niliangazia sana “baadhi tu” ya maeneo ambayo tunakuwa tunayatarajia sana kama ndio sababu kuu sana kuja kutupa maisha mazuri na yenye furaha. Na nikitoa mifano halisi na tafiti mbalimbali ambazo zimewahi kufanyika ulimwenguni kote hasa kuhusu vipengele au vipaumbele ambavyo tumeviweka maishani kwetu kama sababu ya kutufanya tuwe na furaha lakini sio.

(Hakuna kitu nimefundisha na kukiandika kama hakina ushahidi wa kitafiti kutoka kwa wanasaikolojia na wanasayansi)

Basi katika sehemu hii ya pili pia nimeangazia tabia au matendo na mwenendo ambao unaweza kukusaidia kuwa na maisha yenye furaha kama ukusoma sehemu ya kwanza jitahidi upitie ili hiwe na rahisi kwenda pamoja nikirejea ripoti ya taifa la Finland mshindi wa mwaka 2018 kama taifa la watu wenye furaha duniani.

Pia ili huweze kufuatilia vizuri mafundisho haya kuhusu Saikolojia na maisha ni vizuri kama utaanza ni follow katika akaunti yangu “Education mentor”.
Na pia kuhusu Maswali yoyote ya kisaikolojia na maisha unaweza niuliza PM na mimi ntayajibu kwa mfumo wa makala au “mada” kipengele natazamia sana kukianzisha siku za usoni.

 Basi tuendelee katika sehemu ya pili ya kuhusu mada ya “Furaha”
(Kuwa na furaha ni uchaguzi wa mtu katika maisha) 

1.      TABIA YA KUWA NASHUKRANI NA KURIDHIKA. (GRATITUDE AND THANKFULNESS)

(“Kama ukiwa unazingatia katika kutafuta mema na mazuri katika hali zote, basi utagundua maisha yako yanajazwa na moyo wa kuridhika na kushukuru, hisia ambazo zinaistawisha roho yako” Rabbi Kushner)

Hakuna anayependa umasikini (hata mimi sipendi) au hali yoyote kinyume na mtazamo wa jamii kuanzia darasani, kazini na hata katika muonekano wetu mbele ya jamii. Kila mtu anapambana katika maisha kuwa katika hali bora kila leo lakini tunapopambana kuna umuhimu tusiache nyuma “uhalisia” au “uhalisi wetu” kama nilivyoeleza katika sehemu ya kwanza ya makala.

Bado mpaka leo huwa namkumbuka sana binamu yangu katika safari yake ya kutafuta furaha hilipoishia vibaya pasipo matarajio ya familia na wengi tu wakati huo mimi nikiwa bado mdogo sana sijafika hata darasa la 6. Kwa kifupi nina binamu yangu alikuwa kweli kajaliwa “kuwa na akili sana darasani” lakini kuna mtu mmoja ambaye alikuwa anamsumbua sana anashindwa mpita tu yaani yeye alikuwa anakesha na kusoma sana ili hawe mtu wa kwanza lakini hakuwahi kufua dafu ripoti zote za mihula.

Lakini miaka yote hadi kidato cha tatu hakuwahi mpita. Basi kwa kuwa target ya furaha yake aishike nafasi ya kwanza hata mara moja tu. Hivyo akapata watu waliomshawishi akisoma achanganye na bangi kidogo ukweli baada ya hapo akawa mlevi kamili “addicted” tangia hapo hakuweza fikia ndoto zake nyingi na namba mbili darasani akaipoteza na kifupi sina cha kueleza yupo vipi sasa hivi.

Zinavyosema Tafiti.
Wanasaikolojia chanya “Postive Psychology” katika tafiti wanaelezea Kuridhika au kuwa na shukrani ni hali ya kihisia ya kukubali kile ambacho umejaliwa nacho au unacho “moyo wa shukrani”, kinyume na hali ya “nataka-nataka” wakati wote hivyo.
Tafiti bado zinaeleza tunaweza stawisha tabia ya kuridhika na kusaidia kuongeza ubora wetu katika kuyafurahia maisha.
Pia hali ya kuridhika au kuwa na moyo wa shukrani hinausishwa sana katika kuwa na nguvu mitazamo chanya “Optimism” na kuchukuliana na wanadamu wengine.

2.      TABIA YA UKARIMU NA KUJITOA KWA WENYE UHITAJI.
Hiki ni mojawapo ya maswali ambayo yaliulizwa katika utafiti uliotoa ripoti ya taifa la Finland kama watu wenye furaha duniani. Katika tafiti hiyo kulikuwa na swali je humeweza kutoa msaada wowote kwa wahitaji kwa mwezi uliopita?.

(Hakuna tatizo katika kumiliki mali nyingi maishani lakini hakukufanyi kujitosheleza na kila kitu kiini cha utoshelevu ni alama gani nyuma umeacha kwa jamii yako.)

Hapo zamani kidogo kabla sijapata uelewa mara inapotokea kijana anatangulia mbele za haki kwa ghafla mimi huwa ninawahi kuuliza “hivi hajaacha hata mtoto” huku nikisikitika lakini hapo awali sikujua motisha ya swali hili ndani yangu sababu baadae nikagundua watu wengi huuliza hivyo pia.
Unapozungumzia Mwili kumbuka hata wanyama wana miili unapozungumzia roho kumbuka hata wanyama wana roho lakini motisha ya utu wa ndani kwa kundi lote hili ni kuacha vizazi vyetu vikiendelea kuwepo na ndio sababu wengi sana wanaumizwa na suala la ugumba sababu kanuni iliyo ndani ya utu wetu ni kinyume na kutoweka “extinction”. Hii imesaidia sana binadamu tuendelee kuwepo na pia wanyama.

Lakini haitoshi tunaweza kusema kwa kigezo hicho tu ni cha chini sana katika kutuhakikishia “ku survive” kwetu sababu kuna kitu tumewazidi wanyama na hicho ni nafsi (ndani ya nafsi kuna Utashi,Akili na hisia) wanyama hawana nafsi wana roho tu.

Hivyo matendo yote yenye ukarimu na misaada kwa ndugu na jamii inayotuzunguka pasipo mipaka ya sheria, tamaduni, taratibu na  imani zetu ikiwa ina msingi wa utu na upendo wa kuwajari wengine ni sababu kubwa sana ya furaha maishani kwetu usipuuzie hili.
(Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliwahi elezea namna alivyojisikia “fahari” siku alivyopewa nafasi kwa utambulisho wa heshima katika mazishi ya Nelson Mandela (yaliyotazamwa kwa Televisheni karibu ulimwenguni pote). Kutokana na alama “the legacy” aliyoiacha muhasisi wa taifa letu Hayati Mwalimu Nyerere kwa nchi za kusini mwa Afrika, wakati wa harakati za ukombozi dhidi ya ubaguzi wa rangi na ukoloni. Swali Ni namna gani? ulijisikia kuwa Mtanzania siku hiyo <jibu (1)Huzuni au (2)Furaha>).

Kama ulijisikia furaha sana na ufahari kwa mema aliyoyafanya mtu mmoja akiwakilisha taifa zima la watanzania je kwanini na wewe usianze leo kutenda mema na maadili kwa watu waliokuzunguka.
Katika saikolojia kuacha alama “legacy” ni inaeleweka kama nini ntakacho acha nyuma baada ya kufa au ni kumbukumbu zipi nawaachia wanadamu wenzangu baada ya kufa na wanatambua moja ya sababu ya kutafuta kusudi katika maisha ni kumbukumbu utakayoiacha baada ya kundoka katika ulimwengu huu.

3.      KUTUMIA KIPAWA “GIFTEDNESS” AU KARAMA YAKO. 
(Tafiti zinadhibitisha kufanya kazi (zinazohusisha kutumia vipawa vyetu) zinasaidia kutupa furaha na mafanikio katika maisha)

Kipawa maana yake ni nini?  Ni uwezo wa kuzaliwa wa kumwezesha mtu kufanya jambo Fulani. (Kamusi ya karne ya 21, 2011).

Kwa lugha ya kiingereza kipawa ni “talent”, “gift”, “ability”.
Kama ni msomaji wa makala hii ni ambaye ni Mama (Mzazi) tayari. Wakati hupo labor kujifungua. Je wangapi unawakumbuka?. Katika watu waliokuhudumia siku hiyo najua huwezi msahau Nesi aliyekuonesha upendo na kukufariji au daktari aliyekuhudumia kwa upendo siku hiyo.
Kama ni mwanafunzi wa ngazi yoyote kuanzia sekondari hadi chuoni najua huwezi msahau mwalimu aliyejitoa kwako kwa upendo katika kukufundisha.

 Mimi binafsi huwa simsahau mwalimu wangu Mr Ali (Kwa sasa ni mkufunzi chuo kikuu huria “Open University of Tanzania” ) kwa namna alijitoa wakati tupo sekondari hadi kutufuata kule tulipoishi na wenzangu(wakati huo tulipaita “ghetoni”) kutufundisha bila kumlipa chochote kile. na pia muda aliyojitolea wa ziada shuleni kutufundisha masomo ya sanaa darasani nje ya ratiba ya shuleni. Na pia siku hile tulivyofurahia wote matokeo yangu ya kidato cha nne ijapokuwa yalikuwa ya wastani tu lakini alinitia moyo katika safari yangu kwenda vidato vya juu.

Labda ni nini motisha ya ya Daktari, Nesi, Mwalimu au mfanyabishara anayekuhudumia vizuri kwa ukarimu mara unapofika dukani kwake?. Na kwanini kila mtu katika kumbukumbu zake anamuelezea vizuri tu kama wewe unavyomuelezea?.
(“..Kipawa ni kama kito cha thamani” machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa...” Mithali 17:8)
Kuna vitu tunazaliwa navyo kuna ujuzi kipawa karama tunazaliwa navyo kila mmoja ana cha kwake pale tunapoviendeleza au kuvitumia na kugusa jamii zetu kwa namna moja au nyingine kunatupa kufanya kazi pasipo kuchoka wala kutaka kupewa “over time” sababu ndani ya kukufanyika kazi kipawa hicho hipo kufurahia maisha na pasipo tunaowahudumia kujua hilo na wao wanatufurahia wakiita majina ya “ukarimu” na “upendo” pasipo kujua msingi wa furaha nikutumia vipawa vyetu.
Maswali
Je ninaweza fahamu vipi kipawa changu nilichopewa?
Kwanini kazi ninayoifanya inanichosha sana na sina furaha nayo?
Je kinachokufanya uendelee kubaki katika kazi hiyo ni mshahara tu au sababu hauna uamuzi mwingine “other option”?
(makala hii yakuhusu “kipawa” tu naendelea kuiandaa na itakusaidia kufahamu vipawa vyako vilivyopo katika ufahamu wa ndani “Unconscious” kama haujatambua bado)






Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Waelewe Wanaume (Understand Men)

Jifunze mambo yatakayokusaidia kuwa na maisha yenye furaha duniani (Finland Nchi yenye watu wenye furaha duniani?)