Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2018

Mbinu za Kukusaidia kuishi kwa Furaha maishani

Picha
SABABU ZINAZOWEZA KUKUSAIDIA KUKUJENGA NA KUYAFURAHIA MAISHA. Katika sehemu ya kwanza niliangazia sana “baadhi tu” ya maeneo ambayo tunakuwa tunayatarajia sana kama ndio sababu kuu sana kuja kutupa maisha mazuri na yenye furaha. Na nikitoa mifano halisi na tafiti mbalimbali ambazo zimewahi kufanyika ulimwenguni kote hasa kuhusu vipengele au vipaumbele ambavyo tumeviweka maishani kwetu kama sababu ya kutufanya tuwe na furaha lakini sio. (Hakuna kitu nimefundisha na kukiandika kama hakina ushahidi wa kitafiti kutoka kwa wanasaikolojia na wanasayansi) Basi katika sehemu hii ya pili pia nimeangazia tabia au matendo na mwenendo ambao unaweza kukusaidia kuwa na maisha yenye furaha kama ukusoma sehemu ya kwanza jitahidi upitie ili hiwe na rahisi kwenda pamoja nikirejea ripoti ya taifa la Finland mshindi wa mwaka 2018 kama taifa la watu wenye furaha duniani. Pia ili huweze kufuatilia vizuri mafundisho haya kuhusu Saikolojia na maisha ni vizuri kama utaanza ni follow katika ...

Jifunze mambo yatakayokusaidia kuwa na maisha yenye furaha duniani (Finland Nchi yenye watu wenye furaha duniani?)

Picha
Saikolojia: Jifunze mambo yakayokusaidia kuwa na maisha yenye furaha duniani ( na fahamu vigezo vilivyotumiwa kuichagua Finland kuwa nchi ya kwanza (Juu) kwa watu wenye furaha na Tanzania ya tatu (kutoka mwisho). “..Katika makala hii nimejikita kuchambua vigezo vilivyoifanya finland kuwa nchi ya watu wenye furaha kama Case study na kisha kuangazia sababu...”    1.       MWANZO Wanavyoeleza wanafalsafa na wasaikolojia kuhusu dhana ya kuwa na Furaha ni nini? Dhana ya tafsiri kuhusu nini maana ya furaha imejadiliwa sana Duniani kuanzia katika mataifa mbalimbali ulimwenguni kwa watu wa dini, wanafalsafa na mwishoni mwa karne ya 20 ikachipukizia kwa wanasaikolojia mfano William James (1842-1910) “Functionalism school of thought” na Abraham Maslow (1908-1970) wa “ Humanistic School of thought”. i.                     Falsafa Katika Falsafa (Philo...

Je? Nimsamehe au nimlipizie Kisasi?. (Vita visivyoisha vya Afghanistan)

Picha
“.Kabla haujaanza safari ya kwenda kulipa kisasi anza kuchimba makaburi mawili...” Confucius (Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga). Kisasi ni kitu kinachoweka hisia ya ahueni katika mioyo ya binadamu kwa muda, lakini ili kikadiliwe sawasawa na mtendaji wanadamu wamejiekea mifumo mbalimbali ya haki na hukumu ili kusuruhisha au kutoa haki kwa jamii zao. Ili kusudi kuepusha watu kujichukulia sheria mkononi. Lakini ndivyo ulimwengu unavyosema kuhusu kisasi ni sehemu ya maisha ya kila jamii unapotazama maigizo, tamthiliya au kusoma riwaya basi uwa na pande mbili zinazokinzana Mhusika mkuu na adui wa mhusika. Ambapo kama itaanza mhusika mkuu akipitia katika mateso mikononi mwa adui zake au jamii yake ikapitia katika mgogoro huo, basi ili tamthiliya au sinema hiyo iishie ikiwapa tulizo na kufurahisha watazamaji sharti kisasi kilipwe au kutokee kuingilia kati kwa Mungu au miungu kuonesha ikilipa kisasi kwa ad...